Sunday 1 September 2019

TCU: MWISHO WA KUTHIBITISHA CHUO 2019/2020

 Image result for tcu tz

TAARIFA KWA UMMA.

MUDA WA KUTHIBITISHA UDAHILI KWA WALIODAHILIWA ZAIDI YA CHUO KIMOJA MWAKA WA MASOMO 2019/2020.

Tume ya vyuo vikuu Tanzania (TCU), inapenda kuutangazia umma kuwa muda wa kuthibitisha udahili kwa waombaji waliodahiliwa chuo zaidi ya kimoja katika awamu ya kwanza ya udahili mwaka wa masomo 2019/2020 utamalizika siku ya alhamisi tarehe 29/08/2019 saa sita usiku kusoma zaidi bonyeza hapa

Friday 13 April 2018

BARCELONA YAWAOMBA RADHI MASHABIKI WAKE

Tokeo la picha la joseph bartomeu barcelona
Rais wa Barcelona Josep Bartomeu ameomba radhi mashabiki wa klabu hiyo baada ya timu hiyo kutupwa nje katika ligi ya mabingwa Ulaya.
Barcelona iliyokuwa ikipewa nafasi ya kusonga mbele, iliondolewa na AS Roma ya Italia baada ya kuchapwa mabao 3-0 ugenini.
Bartomeu amesema wamepokea kwa masikitiko matokeo hayo na kuwa Roma walikuwa katika kiwango bora uwanjani na walikuwa sahihi kusonga mbele.
Matokeo hayo yanafanya kibarua cha kocha Ernesto Valverde kinaweza kuota mbawa.

Saturday 7 April 2018

China kuchukua hatua ya kulipiza kisasi kwenye mvutano wa kibiashara kati yake na Marekani

Tokeo la picha la china vs usa national flag
Msemaji wa wizara ya biashara ya China Bw. Gao Feng amesema, kama Marekani haitajali upinzani wa China na jumuiya ya kimataifa na kuendelea kufanya vitendo vya upande mmoja na kujilinda kibiashara, China italipiza kisasi bila kujali hasara yoyote, itachukua hatua mpya za mfululizo kukabiliana na hali hiyo, na kulinda kithabiti maslahi ya taifa na wananchi wake.
Rais Donald Trump wa Marekani ametoa taarifa akisema, mwakilishi wa biashara wa Marekani anafikiria uwezekano wa kuongeza ushuru wa ziada wa dola bilioni 100 za kimarekani dhidi ya bidhaa China, huku akiongeza kuwa Marekani bado inataka kufanya mazungumzo.
Bw. Gao amesema, mvutano huo umesababishwa na upande mmoja wa Marekani, ambao uhalisi wake ni upande mmoja wa Marekani kupambana na pande mbalimbali za dunia na hatua ya kujilinda kibiashara ya Marekani inavuruga biashara huria duniani. China itaendelea kupanua mageuzi na ufunguaji wa mlango, kulinda mfumo wa biashara wa pande mbalimbali, kuhimiza uhuru na urahisi wa biashara na uwekezaji duniani.

Tuesday 31 October 2017

TCU:TAARIFA MUHIMU KWA UMMA 2017/2018.

Image result for TCU TZ

TAARIFA KWA UMMA

Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inawatangazia waombaji walioomba kujiunga na masomo ya shahada za kwanza katika Vyuo vya Elimu ya Juu nchini kuwa imekamilisha zoezi la uhakiki wa majina ya waombaji wote walioomba udahili kwa mwaka wa masomo 2017/18.
Hata hivyo Tume imebaini idadi kubwa ya waombaji wamerudia kuomba udahili, wamejithibitisha zaidi ya chuo kimoja au wamechaguliwa katika vyuo zaidi ya kimoja. Waombaji hao wamegawanyika katika makundi matatu:

a) Waombaji waliochaguliwa zaidi ya chuo kimoja katika awamu zote tatu na bado hawajathibitisha KUONA BONYEZA HAPA

b) Waombaji waliothibitisha zaidi ya chuo kimoja KUONA BONYEZA HAPA

c) Waombaji waliokwisha kuthibitishwa vyuoni lakini wakaamua kurudia kuomba upya KUONA BONYEZA HAPA

Tume inaelekeza kwamba;
a) Waombaji walioorodheshwa hapa juu; wanatakiwa kuamua mara moja na kuripoti kwenye chuo kimoja na kufanya usajili katika chuo husika;

b) Tume inasisitiza kuwa waombaji hawa wanatakiwa kuwa wameripoti vyuoni na kusajiliwa kabla ya Tarehe 1 Novemba 2017.

Imetolewa na
Prof. Eleuther Mwageni
Kaimu Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
30 Oktoba 2017


Friday 6 October 2017

NEW: MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU CHA DODOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2017/2018

 Image result for UDOM
Chuo kikuu cha Dodoma kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho kwa mwaka wa masomo 2017/2018,majina haya ni wanafunzi ambao hawajachaguliwa chuo zaidi ya kimoja. KUONA MAJINA BONYEZA HAPA

NEW: MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA ELIMU DAR ES SALAAM(DUCE) 2017/2018

   Image result for duce tanzania                                                                 Image result for UDSM
    Chuo kikuu cha Dar es salaam kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho moja kwa moja yaani majina haya hayajachaguliwa zaidi ya chuo kimoja. Kulingana na wavuti ya chuo kikuu cha Dar es salaam wanafunzi hao wa mwaka wa kwanza wanatakiwa kuanza kuripoti chuo kuchukua admission letter pamoja na kuanza wiki ya utambulisho tarehe 28/10/2017.
MAJINA HAYA NI YA WANAFUNZI WA DUCE CAMPUS,KUYAONA BONYEZA HAPA

NEW: MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDSM) 2017/2018

  Image result for UDSM
 Chuo kikuu cha Dar es salaam kimetoa majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na chuo hicho moja kwa moja yaani majina haya hayajachaguliwa zaidi ya chuo kimoja. Kulingana na wavuti ya chuo kikuu cha Dar es salaam wanafunzi hao wa mwaka wa kwanza wanatakiwa kuanza kuripoti chuo kuchukua admission letter pamoja na kuanza wiki ya utambulisho tarehe 28/10/2017.
MAJINA HAYA NI YA WANAFUNZI WA MLIMANI CAMPUS,BONYEZA HAPA KUYAONA