Monday 26 September 2016

MAN U YAIPA KIPIGO MURUA LEICESTER CITY

Image result for MAN U 
 Manchester United Jumamosi hii imerudisha furaha kwa mashabiki wake na kuzidi kuwazamisha mabingwa watetezi wa Premier League baada ya kupata ushindi wa mabao 4-1, Leicester Cty. United ambayo ilikuwa kwenye Uwanja wa nyumbani, Old Trafford ilionyesha soka safi hasa kipindi cha kwanza na kufanikiwa kuandika mabao yote manne huku nahodha wake, Rooney akianzia benchi.

Image result for leicester city 
 Kwa matokeo haya, United inaongeza alama tatu na hivyo kufikisha jumla ya pointi 12 baada ya kushuka uwanjani mara sita ambapo wamefanikiwa kushinda michezo minne, imepoteza miwili na haijatoa sare. Mabao ya United yalifungwa na: Smalling dakika ya 22; Mata (36), Rashford (39), Pogba (42) huku lile la Leicester likiwekwa kimiani na Gray dakika ya 60.

No comments:

Post a Comment