Wednesday 17 August 2016

ANTONIO CONTE:BADO NINA MIPANGO NA FABREGAS

Image result for fabregas
Kocha wa Chelsea Antonio Conte, amesema kiungo Cesc Fabregas bado ana mipango naye licha ya kutompanga kwenye mchezo wa jana wa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya West Ham, katika uwanja wa Stamford Bridge.
Bao la Costa, kunako dakika ya 89, liliihakikishia Chelsea pointi 3 muhimu, baada ya James Collins, kusawazishia West Ham, wakati Eden Hazard alikuwa ameshaandika bao la kwanza kwa The Blues kwa njia ya peanati.
Fabregas aliyeachwa kwenye benchi, amekuwa akihusishwa na kutaka kutimka kwenye klabu hiyo ya darajani ambapo inasemakana huenda akakimbilia vilabu vya Real Madrid, Juventus au klabu yake ya zamani, Barcelona

No comments:

Post a Comment