Thursday 11 August 2016

WENGER:MATOKEO MSIMU HUU,NDIO HATMA YANGU ARSENAL

Image result for WENGERMeneja wa klabu ya Arsenal ya Uingereza, Arsene Wenger amesema hatma yake katika klabu hiyo ya Emirates inategemea jinsi matokeo ya klabu hiyo msimu huu yatakavyokuwa. Raia huyo wa Ufaransa mwenye miaka 66, aliajiriwa mwezi Septemba 1996 kuiongoza klabu hiyo. Mkataba wake wa sasa utakamilika mwishoni mwa mwezi juni mwaka ujao.
Arsenal haijashinda taji la ligi kuu ya Uingereza tangu mwaka 2004 jambo ambalo limechochea uhasama dhidi ya Wenger haswa kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo. Awali wenger alikuwa amehusishwa na wadhfa wa kocha wa timu ya Uingereza lakini Sam Allardyce akachaguliwa kuchukua nafasi ya Roy Hodgson.

No comments:

Post a Comment